Singida Black Stars yamkomalia mido Mghana

Mwanaspoti
Published: Apr 30, 2026 14:52:39 EAT   |  Sports

UONGOZI wa Singida Black Stars, umeonyesha nia ya kumuhitaji kiungo mshambuliaji wa Gor Mahia ya Kenya, Mghana, Enock Morrison, ambaye hadi sasa hakuna mazungumzo ya kuongeza mkataba mpya huko alipo, pindi uliopo utakapofikia tamati mwisho wa msimu huu.