Mcongo wa Geita aanza tambo
BAADA ya Geita Gold kuinasa saini ya aliyekuwa mshambuliaji wa Namungo FC, ‘Wauaji wa Kusini’, Mkongomani Fabrice Ngoy, nyota huyo ameweka wazi anataka kuendelea kufanya vizuri na kikosi hicho, licha ya ushindani mkubwa wa kuwania nafasi.