Luizer awasihi wanawake kutunza ngozi
MSANII wa muziki wa dansi, Luizer Nyoni Mbutu, amewashauri mabinti na wanawake kuthamini na kutunza ngozi zao kwa kuepuka matumizi ya bidhaa zinazoweza kuathiri afya ya ngozi.
MSANII wa muziki wa dansi, Luizer Nyoni Mbutu, amewashauri mabinti na wanawake kuthamini na kutunza ngozi zao kwa kuepuka matumizi ya bidhaa zinazoweza kuathiri afya ya ngozi. Akizungumza na Daily News Digital, Luizer amesema amewahi kukumbana na changamoto hiyo baada ya kushawishiwa na rafiki yake kutumia bidhaa iliyosababisha ngozi yake kuharibika.
Amesema licha ya kuwa si rahisi kuacha matumizi ya bidhaa hiyo, kwa sasa ngozi yake imeanza kuimarika na kurejea katika hali yake ya awali.Kutokana na uzoefu huo, amewataka wanawake kujipenda na kutokubali shinikizo la kubadilisha mwonekano wa ngozi zao kwa kutumia bidhaa bila kufahamu madhara yake.
“Akili za kuambiwa changanya na zako. Uzuri si kujichubua, ni wewe mwenyewe kukipenda na kuithamini ngozi uliyonayo,” amesema Luizer. Amesisitiza umuhimu wa kuchagua bidhaa salama na kuwa makini na ushauri wanaoupata kuhusu utunzaji wa ngozi. SOMA: Mungu ndiye nguvu ya mafanikio