Ibenge awakomalia mastaa Azam FC

Mwanaspoti
Published: Oct 18, 2025 20:01:27 EAT   |  Sports

LICHA ya Azam kushinda mabao 2-0 katika mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya KMKM, ila kocha wa timu hiyo raia wa DR Congo, Florent Ibenge, amesema hajabweteka na ushindi huo, hivyo bado ana kazi kubwa ya kufanya katika marudiano.