Dili iliyokufa -17
“Hizo taarifa tayari zimesambazwa katika vituo vyote vya polisi. Alama yetu ilikuwa ni namba ya usajili ya hilo gari kwani alipofika hapo gesti, watu waliona namba ya gari alilokuwa nalo. Kwa hiyo ilipotokea hii ajali, polisi walipofika wakaona namba ya usajili ya gari hilo ndiyo namba ya gari ya huyo mtu aliyefanya mauaji”