Coastal Union, TRA United zashindwa kutambiana Mkwakwani
TIMU za Coastal Union na TRA United, zimeshindwa kutambiana katika mechi kali na ya kuvutia ya raundi ya tatu ya Ligi Kuu Bara msimu wa 2026-2027, baada ya miamba hiyo kutoka sare ya kufungana bao 1-1 kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.